Bismillahir Rahmanir Rahim

 

Welcome to

Union of Madrassahs in Dodoma
(UMADO)

Back Home  /  UMADO

MASHINDANO YA KUHIFADHI QURAN TUKUFU

Uongozi wa Umoja Wa Madrassah Dodoma (UMADO) uliandaa kikao Jumamosi tarehe 07/05/2005 ambacho madhumuni yake kilikuwa ni kukutana na walimu wote wa Madrassah juu ya kufanikisha mashindano ya Quran Tukufu kila mwaka. Yafuatayo ndiyo yaliyokubalika katika kikao na yameaanza kufanyiwa kazi rasmi:

 

UMUHIMU WA KUHIFADHI QURAN TUKUFU

 

Hii ni mashindano ya kusoma Quran kwa Hifadhi kwa ajili ya vijana wa Madrassah. Zoezi hili ni muhimu kutokana na hadithi ya Mtume Muhammad (saww) inayosema kuwa: "Hakuna dhambi kubwa kama mtu kuisoma Quran kisha akaisahau". Kutokana na hadithi hii, ni lazima kuandaa mikakati ya kudumu kwa vijana wote wa Madrassah kuhifadhi Quran. Kutokana na umuhimu huu, UMADO imeandaa mikakati kuwashindanisha vijana wa Madrassah katika kuhifadhi Quran kila baada ya miezi sita yaani mara mbili kwa mwaka, na hii kupelekea miaka mitano, mwanafunzi awe amehifadhi mas-hafi yote juzuu thelathini.

 

HIFADHI:

 

Walimu wa Madrassah walipendekeza kuwa kwa hatua ya kwanza, wanafunzi watatakiwa kuhifadhi kwa muundo wa mpangiliowa Quran ilivyopangwa kuanzia Juzu ya 30 na 29.

 

SIFA ZA VIJANA WA MADRASSAH KUSHIRIKI KATIKA MASHINDANO YA QURAN:

    - Umri wowote ila mwisho awe miaka 20.

    - Awe mwanafunzi wa Madrassah.

    - Madrassah iwe imesajiliwa na UMADO.

    - Awe anajua kuisoma Quran kwa hifadhi kuanzia juzu ya 30 na 29.

 

KANUNI ZA MASHINDANO:

  • Msomaji atatakiwa azijue hukumu zote za Quran Tajweed kwa mfano Idgham, Idh-har, Nun  Tanween, Shadda, Madda, Makhraji, n.k.

  • Asome kwa mfululizo bila ya kusita.

  • Usomaji kwa sauti nzuri na ya kupendeza yatakayozingatiwa na majaji.

  • Kuhifadhi kwa msomaji katika maeneo wa Quran kuanzia juzu ya 30 na 29.

  • Majaji wanaweza kuisoma Aya au Sura kwa kifupi kisha msomaji aiendeleze.

 

KUSHIRIKI:

 

Kila madrassah itatoa washindi 2 (1 mvulana na 1 msichana). Ikitokea Madrassah haina msichana wa kushirikisha katika mashindano hayo, basi itabidi uletee wavulana wawili.

Ushiriki utafanyika kikanda yaani Madrassah 10 (kumi) zitakuwa kanda moja. Kuna Madrassah 70 na kanda 7. Kwa hiyo jumla ya kanda saba kutapatikana washiriki 140. Rejea jedwali ya kila Madrassah na kanda yake hapa chini.

 

ZAWADI:

 

Kwa kipindi chote hicho zawadi kubwa zitatolewa, kwa vitu halisi kama cherehani kwa wasichana, baiskeli kwa wavulana, kofia, vitambaa vya kichwani, kanzu na fedha taslimu kadri wafadhili watakavyo changia zoezi hili. Mshindi wa kwanza kwa wavulana atapata Baiskeli na msichana atapata Cherehani. Mshindi wa pili na watatu watapata fedha taslimu. Washiriki wote wengine watapewa zawadi za kushiriki. Aidha na walimu watapewa zawadi zao maalum kutokana na kazi nzuri ya kulisimamia na kuwatayarisha wanafunzi kushiriki katika mashindano haya.

 

WITO:

 

Kikao kilitoa tamko la pamoja kuwa zoezi la kuhifadhi Quran litakuwa la kudumu hivyo linahitaji nguvu za pamoja kwa Waislam wote kushiriki kwa hali na mali. Lengo ni vijana wetu wahifadhi Quran na kuwa na namba nzuri ya wasomaji wa Quran na kuweza kuwafanya wawe tayari kushiriki mashindano nchini na nchi za nje.

 

Asante sana. Wa Billahi Tawfeeq.

 

 

Back Home  /  UMADO