[TAMSA] MOROGORO WARSHA YA VIONGOZI WA
MATAWI UONGOZI WA TAASISI NA
JUMUIYA ZA KIISLAMU IMETAYARISHWA NA: MKOA WA MOROGORO. (MU)

BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIM
MADA: UONGOZI WA TAASISI NA JUMUIYA ZA
KIISLAM
MADHUMUNI: (OBJECTIVES)
Kuwawezesha
washiriki kuwa na mwelekeo, uelewa na stadi muhimu katika kutekeleza jukumu
lao. Kufikiwa hili maudhui inafafanuliwa kwa kutumia mifano halisi sambamba na
kuwa na kazi katika makundi.
MATARAJIO (EXPRECTATIONS)
Inatarajiwa
kuwa washiriki wataweza:
(i)
Kufafanua dhana “uongozi”
(ii)
Kufafanua matumizi stahili ya madaraka ya
uongozi.
(iii)
Kufafanua aina ya mahusiano yanayofaa baina ya
viongozi na wafuasi na hatimaye
kuwezesha
(iv)
Kujitathmini kwa kuzingatia dhana ya uongozi,
madaraka na uhusiano baina ya viongozi na wafuasi
STADI: (SKILLS)
Stadi
zifuatazo zinalengwa.
(i)
Uelewa sahihi kuhusu uongozi.
(ii)
Namna bora ya kuwezesha wafuasi wamkubali
kiongozi na uongozi wake.
IKISIRI (ABSTRACT)
“…..
waulizeni wanojua
1.0 UTANGULIZI
“Uongozi wowote ni sanaa ya kushughulikia masuala ya watu na
kushawishi mwenendo wa
mwanadamu, na kuuongoza mwenendo
huo kuelekea shabaha maalum,
kw namna ambayo itawezesha
kupatikana utii katika hilo, kuwa na imani na
ya yote, heshima kutokana na
kufanya hivyo” (Fathi
Yakan- Tasfsiri)[1]
Kufanikiwa
kwa kiongozi katika dhamira yake, kunategemea
Nafasi
ya kiongozi, mtindo na mchakato wa uongozi ni muhimu, nyeti na tete katika
harakati zozote zile. Kama kiongozi hana sifa zinazotakiwa, na kama mtindo na
mchakato wa uongozi haufai kimsingi na kiutendaji, hakuna shaka kwamba harakati
za taasisi husika zitadorora na kupooza
2.0 MASUALA YA MSINGI
Hakuna
mashaka kwamba taasisi zetu za kiislam ikiwemo TAMSA, zinaongozwa na viongozi, hivyo kwa sababu uongozi ni jambo
la msingi, inafahamika kuwa katika uislam uongozi ni amanah na jukumu ambalo
linapaswa kufanywa kwa uwezo mzuri wa kiongozi. Katika maudhui ya mada hii,
masuala yafuatayo yanaguswa:-
1.
Kwamba kila
mmoja ni mchunga, suala linakuwa “ Je kila mtu ni kiongozi miongoni mwa
wanajumuiya? Je kama ndivyo hivyo nani miongoni mwa wanajumuiya anapaswa kutiiwa
kwanza?
2.
Kwamba uongozi
ni sanaa, ni mchakato na ni fani: Je uelewa huu unanasibiana na mfumo, kanuni
na utendaji wa uongozi wa TAMSA?
3.
Kwamba uongozi ni dhamana, ni amanah na ni dhima : Je viongozi wa TAMSA hususan matawini, wanafanyaje
katika kuzingatia kuwa uongozi ni dhamana, ni amanah na ni dhima? Ni
mimi wasifu wa kiongozi ambaye uongozi wake ni dhamana, ni amanah na ni dhima .
4.
Kwamba ili
kutekeleza jukumu la Uonozi, kiongozi anahitaji madaraka: Je viongozi wa TAMSA watumieje madaraka ili kufanikiwa
kupata ufanisi?
5.
Kuna namna fulani ya uhusiano wa
kiutawala baina ya viongozi na wafuasi ,
suala ni kuwa, hivi namna ya uhusiano wa kiutawala baina ya viongozi wa TAMSA na baina ya viongozi kwa ujumla
na wanaoongozwa inawezesha ufanisi?
3.0 MFUMO WA DHANA
“….. Waulizeni
wanaojua
Waislamu
tumewekewa mfumo na utaratibu mzuri kimaisha katika kila kipngele. Katika mfumo
wa kijamii waislam tunatakiwa kuwauliza wanaojua ikiwa hatujui. Bila shaka
warsha hii ni mazingira ya kutekeleza mafundisho ya aya hii. Katika kufanya hivyo
tuanangalia dhana za uongozi
3.1 Maana ya Uongozi
Uongozi
ni mchakato ambao kwao, kiongozi anatfuta ushiriki wa wafuasi kwa hiyari
Kwa
kuzingtia sifa na nafasi ya kiongozi katika mafanikio ya taasisi, asasi,
Jumuiya au kikundi ama harakati, ni rahisi kuona kuwa uongozi si tu ni mchakato,
bali pia ni sanaa, ni ujuzi na uongozi ni fani. Kwa kifupi fasili zifuatazo
zinatoa uelewa kuhusu Uongozi.
(i)
Uongozi
ni sanaa kwa vile unahitaji uzuri na kupendeza katika mikabala
(approaches). Unahusu ustadi wa kiongozi katika kuwashawishi na kuwalekeza
watu.
“Hakuna
kulazimishana katika dini” (Q. 2:256)
Aya
hii inatuonyesha dhahiri kuwa kiongozi anapaswa kuwa na uwezo wa kubuni na
kuyaweka maono katika vitendo vya wafuasi katika mtindo wa kushawishi. Uwezo
huu ni snaa. Kwa hiyo utaalamu, umahiri na umilisi unahitajika.
(ii)
Uongozi
ni mchakato kwa kuwa unahitaji kupitia hatua na ngazi
kadhaa katika kushwishi na kupata ushiriki wa wafuasi. Kwa sababu hiyo kuongoza
siyo kushawishi mara moja na kusubiri matokeo ya ushawishi.
(iii)
Uongozi
ni fani maalum kwa kuwa zipo kanuni, ipo misingi na yapo maadili
maalum. Kwa kufuata na kuzingatia kanuni na misingi ya uongozi wa kiislamu
(iv)
Uongozi
ni kundi la watu wanaozindua na kuwAtumikia wafuasi, kwa
kuonyesha njia na mwelekeo kIsha kuwashawishi wafuasi wafuate njia hiyo.
(v)
Uongozi ni utaratibu uliopo wa kutumia sanaa katika
mchakato wa kuwawezesha watu kufika katika malengo yaliyowekwa.
3.2 Haja na nafasi ya uongozi katika Jumuiya
na Taasisi
Kwa
kuzingatia fasili ya uongozi, iwe
mchakato, sanaa au fani na hata kundi la watu, ni rahisi kueleza haja ya
uongozi na kueleweka. Katika mafundisho
ya uislam, uongozi si suala la hiyari, bali ni suala la lazima. Kila wawapo
wawili au zaidi, uislamu umeelekeza kuwa lazima
awepo kiongozi. Hii maana yake ni kuwa kila penye watu, uongozi ni
lazima. Suala litabaki juu ya aina ya uongozi.
Katika
kutekeleza mafundisho ya uislamu kuhusu uongozi, viongozi wanapaswa kukumbuka
kuwa:-
(i)
Uongozi ni dhamana
(ii)
Uongozi ni dhima
(iii)
Uongozi ni amanah.
Pamoja
na hayo, kutokuwa na uongozi ni kujikaribisha kwa shaitwan.
Al- hadith
“Kila
mmoja wenu ni mchunga na kila mcunga ataulizwa
juu ya kile alichokichunga” [4]
Tukiitafakari hadithi hii kwa kina , tunajifunza
kuwa pamoja na kuwa na uongozi, wanaoongozwa pia, wanalo jukumu la kuhakiisha
kuwa hakuna uongozi mbovu watu wajue kuwa wataulizwa juu ya
walichokidhunga. Iwapo ummah, Jumuiya,
taasisi au asasi itakuwa na uongozi mbovu, kila mwanjumuiya atakuwa mas’ulia.
3.3 Dhima ya Uongozi
Dkt.
Jamal Badawi, profesa na mwenyeit wa menejiment na stratejia, katia Chuo kiku
cha
(i)
Utumishi kwa anaowaongoza.
(ii)
Ulinzi wa wafuasi dhidi ya ukandamizaji
Dhima
hii nayo imesisitizwa na mtume (s.a.w). kwamba
kiongozi anapaswa kuwalinda wafuasi wake dhidi ya ukatili uonezi na
ukandamizaji vile vile kiongozi anapaswa kuwezesha umaizi kuhusu Mungu , taq’wa
na haki.[7]
(iii)
Ulezi wa wafuasi
Dhima
nyingine muhimu ni ulezi. Ukiwa kiongozi
unailea jumuiya, unawalea wafuasi, unailea
taasisi, unailea asasi. Jukumu la ulezi ni muhimu
4.0 MADARAKA YA KIONGOZI
Dhana
ya madaraka katika muktadha huu ni uwezo wa kupanga, kuratibu, tumia rasilimali
watu, taarifa au habari, na fedha, kufanya
mambo ya jumuiya, taasisi au asasi, yaene
4.1 Madaraka
kutokana na wadhifa (Legistrate
power)
Madaraka
aliyonayo mtu kutokna na wadhifa katika taasisi. Kwa ujumla uislam haupendekezi
waislam kuwa na uamilifu wa kampeni ya kuwatafuta nafasi ya mamlaka. Kwa
muislam kufanya kampeni ili apate wadhifa ambao utampa kampeni ili apate
wadhifa ambao utampa madaraka, ni ishara ya kuwa mtu huyo anatamaa ya wadhifa
kwa maslahi yake binafsi.
Al- hadith
“
Usiombe uongozi kwa sababu
utakapopewa uongozi
kutokana na kuomba, utaachiwa
pekee yako (bila msaada
wa Allah kutekeleza jukumu na wajibu
unaonasibiana nao)
Na kama umepewa uongozi bila
kuomba, utasaidiwa
(Na Allah katika utekelezaji wa majukumu
yako).[9]
4.2 Madaraka kutokana na uwezo wa kuzawadia.
Kiongozi
ambaye anatawala rasilimali za ummah, jamii au taasisi, anaweza pia kuwa na
uwezo wa kuzawadia kutokana na mamlaka na wajibu wkae. Maelezo haya ni sahihi pia katika mafundisho ya
uislam.[10]
Inapendeza kusikia kuwa Seyyid na Umar Ibn Khatb[11]
(r.q) alikuw aakiwalipa mishahara ya juu, maadisa wa dola ya kiislam. Alifanya
hivyo ili kuhakikisha kuwa hawashawishiki kupokea rushwa. Kwa kuwajali
aliwateua
Matumizi
sahihi ya madaraka haya yanawezesha mafanikio na uamilifu wa jumuiya na taasisi
au asasi za kiislamu
4.3 Madaraka ya kinguvu (Coeraive power)
Kwa
kuwa na mamlaka ya kiuonogzi, kiongozi anao uwezo wa kuadhibu kwa niaba ya
anaowaongoza na pia kwa maslahi ya anaowaongoza. Uislamu unatambua kuswihi kwa madaraka
haya, lakini unafundisha kuwa madaraka haya yasitumike kuwafanya wafuasi
kufanya uovu. Ni kwa ukweli huu Mtume (s.a.w) anayesema kuwa “ Utii (kwa
kiongozi) unatakiwa kwa lile tu lililo jema.[12]
Katika kusisitiza dhima ya kiongozi wa kiislam na matumizi mazuri ya madaraka
ya kinguvu, seyydina Umar (r.a) alinukuliwa akiwaambia watu:
“ Nimekuteulieni
magavana na mawakala, siyo kuwaadhibu au
kuchukua
fedha zetu bali kuwfundisha na kuwatumika. [13]
4.4 Madaraka kwa utaalamu (Expart power)
Kwa
kawaida kiongozi mwenye uelewa, maarfia, ujuzi na habari au taarifa muhimu,
anayo madaraka kitaalamu. Anao uwezo wa kuwafanya wafuasi watekeleze jukumu fulani
kwa mpangilio mzuri na kwa namna sahihi pasipo vikwazo.
Mfano:-
Katika
swala ya Jumaa mtu anapaswa kuchaguliwa kuwaongoza wanaosali, kwa kigezo cha
ujuzi na maarifa yake juu ya swala. Kutokana na utaalam alionao imam, maamuma
watamfuata katika utartibu mzima wa swala. Uwezo huu alionao Imam katika
wafanya maamuma wafuate ni madaraka kwa utaalamu juu ya swala.
Mfano
mwingine ni juu ya uweo wa Amir wa Da’awah kuwafanya wanajumuiya kufuata maelezo
yake kutokana na hakika kuwa Amir huyo anayo maarifa juu ya
5.0 MISINGI YA MAADILI YA UONGOZI WA KIISLAM
Kwa
sababu kuongoza ni kutekeleza maamrisho ya Allah(s.w) na mafundisho ya mutume
(s.a.w) na kwa kuwa kuongoza pia ni kufanya ibada, basi kiongozi anapaswa
kutekeleza majukumu na wjaibu wa
maelekezo ya Quran na Sunnah pamoja na
kujikita katika Akhlaq ya kiislam (Islamic Moral character). Akhlaq ya Kiislam
inakuwa madhubuti kadiri mja anavyoongeza uthabiti katika kumuamini Mwenyezi
Mungu kupitia hatua nne za kiroho.
5.1 Iman
Ni kuamini kwa dhati juu ya kuwa mwenyezi Mungu ni momoja ( Tawhid). Kwa kuwa na Imani, kiongozi atajielewa kuwa yeye na vilivyo chini yake, vinamilikiwa na Allah(S.w). Pia Iman inamkumbusha kiongozi juu ya akhera na umas’uulia (Accoutability). Kwa hiyo Iman inamkumbusha kiongozi kuwajibika. Katika kukazia hili, Quran imetaja na kuhusianisha Iman na amali njema si chini ya mara 60