TANZANIA MUSLIM STUDENTS ASSOCIATION

[TAMSA]

 

                                       MOROGORO

 

 

WARSHA YA VIONGOZI  WA  MATAWI

 

 

 

 

 

 

UONGOZI WA TAASISI NA JUMUIYA ZA KIISLAMU

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

IMETAYARISHWA NA:

 

MKOA WA MOROGORO.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

(MU)

 

 


 

BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIM

TANZANIA MUSLIM STUDENTS ASSOCIATION

 

MADA: UONGOZI WA TAASISI NA JUMUIYA ZA KIISLAM

MADHUMUNI: (OBJECTIVES)

Kuwawezesha washiriki kuwa na mwelekeo, uelewa na stadi muhimu katika kutekeleza jukumu lao. Kufikiwa hili maudhui inafafanuliwa kwa kutumia mifano halisi sambamba na kuwa na kazi katika makundi.

 

MATARAJIO (EXPRECTATIONS)

Inatarajiwa kuwa washiriki wataweza:

(i)                  Kufafanua dhana “uongozi” kama mchakato, fani na sanaa.

(ii)               Kufafanua matumizi stahili ya madaraka ya uongozi.

(iii)             Kufafanua aina ya mahusiano yanayofaa baina ya viongozi na wafuasi  na hatimaye kuwezesha hilo.

(iv)              Kujitathmini kwa kuzingatia dhana ya uongozi, madaraka na uhusiano baina ya viongozi na wafuasi

STADI: (SKILLS)

Stadi zifuatazo zinalengwa.

(i)                  Uelewa sahihi kuhusu uongozi.

(ii)               Namna bora ya kuwezesha wafuasi wamkubali kiongozi na uongozi wake.

IKISIRI (ABSTRACT)

“….. waulizeni wanojua kama hamjui” (22:41)

 

 Ili kutekeleza maelezo ya ayah hii, kuna haja ya kuwa na mazingira yanayowezesha kubadilishana uzoefu. Warsha na semina ni miongoni mwa mazingira hayo. Katika mada hii dhana ya uongozi imeelezwa. Mengine yaliyoelezwa ni dhima ya uongozi, madaraka ya uongozi, misingi ya maadili ya uongozi, madaraka ya uongozi, misingi ya maadili ya uongozi, wasifu wa kiongozi wa kiislamu, pamoja  na  uhusiano baina ya viongozi na wafuasi. Hoja katika mada hii ni kwamba ufanisi wa kiongozi unategemea sana matumizi ya madaraka, maadili ya kiongozi, na wasifu wake kiongozi.

 

 

 

 

 

 

 

1.0 UTANGULIZI

“Uongozi wowote ni sanaa ya kushughulikia  masuala ya watu na

kushawishi mwenendo wa mwanadamu, na kuuongoza mwenendo

huo kuelekea shabaha maalum, kw namna ambayo itawezesha

 kupatikana utii katika hilo, kuwa na imani na hilo na zaidi

ya yote, heshima kutokana na kufanya hivyo” (Fathi Yakan- Tasfsiri)[1]

 

Kufanikiwa kwa kiongozi katika dhamira yake, kunategemea sana sifa na uwezo alionao. Hata hivyo hatupaswi kusahau kuwa kuna vipawa vya asili alivyonavyo kiongozi, vinavyompa uwezo wa kufanikiwa katika uongozi, lakini si kwa kiasi kikubwa sana, Haiba (Personality) ya kiongozi hujazilizwa na sifa  nyingine kama vile zile za kiitikadi, kiroho, kiumbile, kiutawala kimaadili na wasifu wa mwenendo wa mtu.

 

Nafasi ya kiongozi, mtindo na mchakato wa uongozi ni muhimu, nyeti na tete katika harakati zozote zile. Kama kiongozi hana sifa zinazotakiwa, na kama mtindo na mchakato wa uongozi haufai kimsingi na kiutendaji, hakuna shaka kwamba harakati za taasisi husika zitadorora na kupooza kama sio kifo cha Jumuiya na taasisi hiyo.

 

2.0 MASUALA YA MSINGI

Hakuna mashaka kwamba taasisi zetu za kiislam ikiwemo TAMSA, zinaongozwa na viongozi, hivyo kwa sababu uongozi ni jambo la msingi, inafahamika kuwa katika uislam uongozi ni amanah na jukumu ambalo linapaswa kufanywa kwa uwezo mzuri wa kiongozi. Katika maudhui ya mada hii, masuala yafuatayo yanaguswa:-

 

1.      Kwamba kila mmoja ni mchunga, suala linakuwa “ Je kila mtu ni kiongozi miongoni mwa wanajumuiya? Je kama ndivyo hivyo nani miongoni mwa wanajumuiya anapaswa kutiiwa kwanza?

2.      Kwamba uongozi ni sanaa, ni mchakato na ni fani: Je uelewa huu unanasibiana na mfumo, kanuni na utendaji wa uongozi wa TAMSA?

3.      Kwamba uongozi ni dhamana, ni amanah na ni dhima : Je viongozi wa TAMSA hususan matawini, wanafanyaje katika kuzingatia kuwa uongozi ni  dhamana, ni amanah na ni dhima? Ni mimi wasifu wa kiongozi ambaye uongozi wake ni dhamana, ni amanah na ni dhima .

4.      Kwamba ili kutekeleza jukumu la Uonozi, kiongozi anahitaji madaraka: Je viongozi wa TAMSA watumieje madaraka ili kufanikiwa kupata ufanisi?

5.      Kuna namna fulani ya uhusiano wa kiutawala  baina ya viongozi na wafuasi , suala ni kuwa, hivi namna ya uhusiano wa kiutawala baina ya viongozi wa TAMSA na baina ya viongozi kwa ujumla na wanaoongozwa inawezesha ufanisi?

 

3.0 MFUMO WA DHANA

“….. Waulizeni wanaojua kama ninyi  hamjui” (Q. 22:41)

 

Waislamu tumewekewa mfumo na utaratibu mzuri kimaisha katika kila kipngele. Katika mfumo wa kijamii waislam tunatakiwa kuwauliza wanaojua ikiwa hatujui. Bila shaka warsha hii ni mazingira ya kutekeleza mafundisho ya aya hii. Katika kufanya hivyo tuanangalia dhana za uongozi kama zilivyoelezwa na wanachuoni kadha.

 

3.1 Maana ya Uongozi

Uongozi ni mchakato ambao kwao, kiongozi anatfuta ushiriki wa wafuasi kwa hiyari yao, katika jitihada za kuyaelendea malengo fulani.[2] Aidha tuanweza pia kusema kwamba uongozi ni mchakato wa kuwaelekeza watu na kuwashawishi katika utendaji pasipo kutumia mabavu.[3]

 

Kwa kuzingtia sifa na nafasi ya kiongozi katika mafanikio ya taasisi, asasi, Jumuiya au kikundi ama harakati, ni rahisi kuona kuwa uongozi si tu ni mchakato, bali pia  ni sanaa, ni ujuzi na  uongozi ni fani. Kwa kifupi fasili zifuatazo zinatoa uelewa kuhusu Uongozi.

 

(i)                  Uongozi ni sanaa kwa vile unahitaji uzuri na kupendeza katika mikabala (approaches). Unahusu ustadi wa kiongozi katika kuwashawishi na kuwalekeza watu.

“Hakuna kulazimishana katika dini” (Q. 2:256)

 

Aya hii inatuonyesha dhahiri kuwa kiongozi anapaswa kuwa na uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo vya wafuasi katika mtindo wa kushawishi. Uwezo huu ni snaa. Kwa hiyo utaalamu, umahiri na umilisi unahitajika.

 

(ii)               Uongozi ni mchakato kwa kuwa unahitaji kupitia hatua na ngazi kadhaa katika kushwishi na kupata ushiriki wa wafuasi. Kwa sababu hiyo kuongoza siyo kushawishi mara moja na kusubiri matokeo ya ushawishi.

(iii)             Uongozi ni fani maalum kwa kuwa zipo kanuni, ipo misingi na yapo maadili maalum. Kwa kufuata na kuzingatia kanuni na misingi ya uongozi wa kiislamu kama inavyoelezwa katika Quran na Sunnah, mtu atafanikiwa katika matumizi ya fani hii ya uongozi.

(iv)              Uongozi ni kundi la watu wanaozindua na kuwAtumikia wafuasi, kwa kuonyesha njia na mwelekeo kIsha kuwashawishi wafuasi wafuate njia hiyo.

(v)                 Uongozi ni utaratibu uliopo wa kutumia sanaa katika mchakato wa kuwawezesha watu kufika katika malengo yaliyowekwa.

 

3.2 Haja na nafasi ya uongozi katika Jumuiya na Taasisi

Kwa kuzingatia fasili   ya uongozi, iwe mchakato, sanaa au fani na hata kundi la watu, ni rahisi kueleza haja ya uongozi  na kueleweka. Katika mafundisho ya uislam, uongozi si suala la hiyari, bali ni suala la lazima. Kila wawapo wawili au zaidi, uislamu umeelekeza kuwa lazima  awepo kiongozi. Hii maana yake ni kuwa kila penye watu, uongozi ni lazima. Suala litabaki juu ya aina ya uongozi.

Katika kutekeleza mafundisho ya uislamu kuhusu uongozi, viongozi wanapaswa kukumbuka kuwa:-

(i)                  Uongozi ni dhamana

(ii)               Uongozi ni dhima

(iii)             Uongozi ni amanah.

 

Pamoja na hayo, kutokuwa na uongozi ni kujikaribisha kwa shaitwan.

                         Al- hadith

“Kila mmoja wenu ni mchunga na kila mcunga ataulizwa

 juu ya kile alichokichunga” [4]

 

Tukiitafakari hadithi hii kwa kina , tunajifunza kuwa pamoja na kuwa na uongozi, wanaoongozwa pia, wanalo jukumu la kuhakiisha kuwa hakuna uongozi mbovu watu wajue kuwa wataulizwa juu ya walichokidhunga.   Iwapo ummah, Jumuiya, taasisi au asasi itakuwa na uongozi mbovu, kila mwanjumuiya atakuwa mas’ulia.

 

3.3 Dhima ya Uongozi

Dkt. Jamal Badawi, profesa na mwenyeit wa menejiment na stratejia, katia Chuo kiku cha Nevada, alisema kwmba katika uislam dhima mbili za uongozi katika uislamu ni:-

 

 

 

(i)                  Utumishi kwa anaowaongoza.

Kwanza, kiongozi ni mtumishi wa anaowaongoza (sayyid al qawan khadimuhum) anapaswa kuwatafutia ustawi bora na kuwaongoza katika mema.[5] Dhana kwmba kiongozi ni mtumishi wa anaowaongoza ni sehemu ya uislamu tangu kwanza kwa uislamu. Kiongozi anayezingatia dhima hii anachukua nafasi ya utumishi kwanza. Suala la muhimu kujiuliza, ni kwa kiwango gain kiongozi  wa taasisi,  jumuiyah na Harakati za Kiislamu wanajiuliza kuhusu dhamira yao ya utumishi au ni viongozi pasiopo dhamira hii ya utumishi. Tukumbuke kuwa “mkuu wa ummah ndiye khadimu wao”[6]

 

(ii)               Ulinzi wa wafuasi dhidi ya ukandamizaji

Dhima hii nayo imesisitizwa na mtume (s.a.w). kwamba  kiongozi anapaswa kuwalinda wafuasi wake dhidi ya ukatili uonezi na ukandamizaji vile vile kiongozi anapaswa kuwezesha umaizi kuhusu Mungu , taq’wa na haki.[7]

 

(iii)             Ulezi wa wafuasi

Dhima nyingine  muhimu ni ulezi. Ukiwa kiongozi unailea jumuiya, unawalea wafuasi, unailea  taasisi, unailea asasi. Jukumu la ulezi ni muhimu sana katika jamii. Mara zote kiongozi unapaswa kuwaza namna ya kuifanya Jumuiya yako ikue, ikomae, ifanikiwe, itosheke, iridhike, iendelee, ijiimarishe and kujijenga katika maisha ya ki- taasisi pamoja na kufanikiwa katika madhumuni yake. Kwa maelezo hayo, iwe kiongozi ni mlezi, mlinzi au mtumishi bila shaka atahitaji madaraka. Uislamu unayatambua madaraka ya kiongozi.

 

4.0 MADARAKA YA KIONGOZI

Dhana ya madaraka katika muktadha huu ni uwezo wa kupanga, kuratibu, tumia rasilimali watu, taarifa au habari, na fedha,   kufanya mambo ya jumuiya, taasisi au asasi, yaene kama inavyotakiwa.[8] Kama kiongozi atakosa uwezo huu, atadorora na  jumuiya, jamii, ummah au taasisi anayoiongoza itakuwa duavu (inactive). Kuna namna nyingi za kueleza madaraka kwa kuzingatia sunnah and Quran.

 

4.1 Madaraka kutokana na wadhifa (Legistrate power)

Madaraka aliyonayo mtu kutokna na wadhifa katika taasisi. Kwa ujumla uislam haupendekezi waislam kuwa na uamilifu wa kampeni ya kuwatafuta nafasi ya mamlaka. Kwa muislam kufanya kampeni ili apate wadhifa ambao utampa kampeni ili apate wadhifa ambao utampa madaraka, ni ishara ya kuwa mtu huyo anatamaa ya wadhifa kwa maslahi yake binafsi.

                          Al- hadith

“ Usiombe uongozi kwa sababu utakapopewa  uongozi

kutokana na kuomba, utaachiwa pekee yako (bila msaada

 wa Allah kutekeleza jukumu na wajibu unaonasibiana nao)

Na kama umepewa uongozi bila kuomba, utasaidiwa

 (Na Allah katika utekelezaji wa majukumu yako).[9]

 

4.2 Madaraka kutokana na uwezo wa kuzawadia.

Kiongozi ambaye anatawala rasilimali za ummah, jamii au taasisi, anaweza pia kuwa na uwezo wa kuzawadia kutokana na mamlaka na wajibu wkae. Maelezo  haya ni sahihi pia katika mafundisho ya uislam.[10] Inapendeza kusikia kuwa Seyyid na Umar Ibn Khatb[11] (r.q) alikuw aakiwalipa mishahara ya juu, maadisa wa dola ya kiislam. Alifanya hivyo ili kuhakikisha kuwa hawashawishiki kupokea rushwa. Kwa kuwajali aliwateua kama ilivyostahiki, Seyyidna Umar (r.a) akawa kiongozi mashuhuri na aliyefanikiwa. Na kwa namna hiyo, Seyyidna Umar (r.a) ni mfano wa kuigwa na watawala katika ulimwengu leo na pia ni mfano wa kuigwa na  watawala katika ulimwengu leo na pia ni mfano wa kuigwa na viongozi wa jumuiya ya taasisi za kiislam.  Matumizi sahihi ya madaraka haya yanawezeshs mafanikio na uamilifu wa Jumuiya  na taasisi au asasi za kiislamu.

 

Matumizi sahihi ya madaraka haya yanawezesha mafanikio na uamilifu wa jumuiya na taasisi au asasi za kiislamu

 

4.3 Madaraka ya kinguvu (Coeraive power)

Kwa kuwa na mamlaka  ya  kiuonogzi, kiongozi  anao uwezo wa kuadhibu kwa niaba ya anaowaongoza na pia kwa maslahi ya anaowaongoza. Uislamu unatambua kuswihi kwa madaraka haya, lakini unafundisha kuwa madaraka haya yasitumike kuwafanya wafuasi kufanya uovu. Ni kwa ukweli huu Mtume (s.a.w) anayesema kuwa “ Utii (kwa kiongozi) unatakiwa kwa lile tu lililo jema.[12] Katika kusisitiza dhima ya kiongozi wa kiislam na matumizi mazuri ya madaraka ya kinguvu, seyydina Umar (r.a) alinukuliwa akiwaambia watu:

 

“ Nimekuteulieni magavana na mawakala, siyo kuwaadhibu au

kuchukua fedha zetu bali kuwfundisha na kuwatumika. [13]

 

4.4 Madaraka kwa utaalamu (Expart power)

Kwa kawaida kiongozi mwenye uelewa, maarfia, ujuzi na habari au taarifa muhimu, anayo madaraka kitaalamu. Anao uwezo wa kuwafanya wafuasi watekeleze jukumu fulani kwa mpangilio mzuri na kwa namna sahihi pasipo vikwazo.

Mfano:-

Katika swala ya Jumaa mtu anapaswa kuchaguliwa kuwaongoza wanaosali, kwa kigezo cha ujuzi na maarifa yake juu ya swala. Kutokana na utaalam alionao imam, maamuma watamfuata katika utartibu mzima wa swala. Uwezo huu alionao Imam katika wafanya maamuma wafuate ni madaraka kwa utaalamu juu ya swala.

 

Mfano mwingine ni juu ya uweo wa Amir wa Da’awah kuwafanya wanajumuiya kufuata maelezo yake kutokana na hakika kuwa Amir huyo anayo maarifa juu ya hilo.

 

5.0  MISINGI YA MAADILI YA UONGOZI WA KIISLAM

Kwa sababu kuongoza ni kutekeleza maamrisho ya Allah(s.w) na mafundisho ya mutume (s.a.w) na kwa kuwa kuongoza pia ni kufanya ibada, basi kiongozi anapaswa kutekeleza  majukumu na wjaibu wa maelekezo ya Quran  na Sunnah pamoja na kujikita katika Akhlaq ya kiislam (Islamic Moral character). Akhlaq ya Kiislam inakuwa madhubuti kadiri mja anavyoongeza uthabiti katika kumuamini Mwenyezi Mungu kupitia hatua nne za kiroho.

5.1  Iman

Ni kuamini kwa dhati juu ya kuwa mwenyezi Mungu ni momoja ( Tawhid). Kwa kuwa na Imani, kiongozi atajielewa kuwa yeye na vilivyo chini  yake, vinamilikiwa na Allah(S.w). Pia Iman inamkumbusha kiongozi juu ya  akhera na umas’uulia (Accoutability). Kwa hiyo Iman inamkumbusha kiongozi kuwajibika. Katika kukazia hili, Quran imetaja na kuhusianisha Iman na amali njema si chini ya mara 60[14]

 

Mfano wa Sahaba, Amr Ibn Al Aas, aliteuliwa na mtume (s.a.w) katika uongozi, takriban miezi mine tu baada ya kuingia katika uislam. Habari hii inaweza kuthibitishwa kwa akusoma kitabu kilichoandikwa na Ibn Taymiyya kiitwacho ASSIYAH ASH- SHAR ‘IYYA.

 

5.2  Islam

Ni sehemu muhimu pia katika haiba na maadili ya kiongozi wa kiislamu. Isam  hapa inamaana kujisalimisha kwa  mwenyezi Mungu na pia kuwa na amani baina ya mja na viumbe wa Allah (s.w), kwa njia ya kunyenyekea kwa Allah.[15]

“ Iman ni mbegu na Islam ni mafanikio ya Iman[16]

Kiongozi mwenye Iman anapotekeleza jukumu la uongozi wake katika uislam, hathubutu kujitukuza wala hatajaribu kujiona kuwa mbora zaidi ya wote na kila kitu.

 

Imam Ali Ibn Abutalib (r.a) aliandika barua kwa Malik  al – Ashtar an – Nukai, gavana mpya wa Misri akishadidisha hoja hii.

 

                                     “ Malik; unalazimika kutosahau kwamba kama wewe ni

   mtawala/ kionogzi wao, basi khalifa ni kiongozi wako

   na mwenyezi Mungu ni juu ya khalifa[17]

 

5.3  Taqwa

Hii ni hisia ya heshima na uelewa vikichanganyika na kumuogopa Mwenyezi Mungu. Kwa kuwa na Taqwa, kiongozi anakuwa na umaizi (consciousness) kuhusu jukumu lake kwa Allah (sw). Kwa kuwa na taqwa, kionogzi anakuwa hadhir na uma’swulia wake kwa Mwenyezi Mungu.

 

“Msingi wa taqwa upo katika mtizamo w amoyo na akili

kuliko muonekano wa nje

 

Kwa hiyo taqwa inamfanya kiongozi anakuwa na mkao wa akili, fikra, hisa na maono yanayoakisi uislam. Kwa sababu hiyo, uongozi wa kiongozi huyo utaendana na amali njema.

 

                         “ kwa hakika Mwenyezi Mungu anaamrisha uadilifu na

                        kufanya hisani, na kuwapa jamaa (na wengineo): na

                         anakataza uchafu na uovu na dhuluma. Anakunasihini

                         ili mpate kufahamu (mfuate).” (An nahl)[18]

 

5.4  Ihsan

Wakati taqwa inahusisha kumwoogopa Allah (sw) na kuwa na hisa juu ya kuwepo kwake, Ihsan ni Kumpenda Mwenyezi Mungu. Ihsani inamfanya kiongozi kuwa na juhudi katika kumridhisha Allah. Jitiahda hii itamfanya kiongozi kutekeleza wajibu wake ipasavyo na kuifanya taasisi au Jumuiya ya kiislam kufanikiwa kwa kufuata misingi ya Quran na Sunnah.

 

 Al- hadith

“ Ihsan ni kumwabudu Mwenyezi Mungu kana kwmba

 Unamwona. na kama huwezi kufikia hali hii unapaswa

Kujaalia kuwa anakutazama.”[19]

 

Kiongozi kuwa na Ihsan, ataongoza kwa uadilifu na kwa dhamira stahiki, mambo ambayo yatawezesha ufanisi wa Jumuiya na  mafanikio ya jumuiya kwa ujumla kwa mnasaba wa madhumuni ya jumuiya na Taasisi ya kiislam.

 

 

 

6.0  WASIFU WA KIONGOZI WA KIISLAM

Ili kiongozi aweze kuongoza kwa ufanisi kuna wasifu maalum anaopaswa kuwanao. Yapo mambo kadhaa ya kuzingatiwa katika kuweza kuwa na wasifu huo, mionogni mwa mengi ni pamoja na:-

6.1  Elimu na Hikmah

 

“ Ee Mola wetu! Waletee Mtume anayetokana na wao, awasomee

 Aya zako na kuwafundiaha kitabu (chako) na hikma (nyingine)

 na wafundishe kujitakasa (na kila mabaya) …” (Al- Baqara, 2:129 )

 

 

         “Mfano wa wale waliopewa Taurati, kisha hawa kuichukua

          (kutumia) ni kama punda anayebeba vitabu vikubwa (bila kupata

         nafuu kwavyo). Ni m- baya kabisa mfano wa watu waliozikadhibisha

         Aya za MwenyeziMungu;  na Mwenyezi Mungu hawaogopi

          madhalimu” (AL- Jumla, 62:05)

 

Aya hizi zinaonyesha umuhimu wa Elimu na Hekma kwa kiongozi vinginevyo kiongozi huyo ni sawa na punda aliyebeba vitabu. Aidha katika aya hizo na nyingine kadha, zinaonesha kuwa Mtume (s.a.w) alipewa maarifa na hekmah ili aweze kufanikisha mafundisho ya uislam katika ummah waka. Mazingatio tunayopata hapa ni kuwa: kwa kuwa kiongozi wa kiislam anao wajibu kwa ummah, matumzi ya hekma ni muhimu. Kiongozi anapaswa kutumia vema madaraka yake katika kufanya maamuzi yanayoathiri jumuiya, jamii, ummah na taasisi, maamuzi ya kiongozi yafanywe kwa hekma.

 

Kuna mifano mingi katika Seerah ya Mtume (s.a.w) ambapo hekma yake ilizaa matunda japokuwa baadhi ya masahabaa hawakuwa wameweza kuigundua mapema . Mfano mzuri wa hoja hii unadhihiri katika mkataba wa Hudaibiyya mwaka wa 6 Hijiria[20]

 

6.2  Adl na Rahma

                   Adl na Rahmah ni mambo mawili muhimu sana kwa kiongozi.

 

                                    “ Adl bila Rahmah husababisha ukatili wakati Rahmah bila Adl huzaa

                        mkanganyiko na Mkorogo (disorder)” [21]

 

   Kiongozi anapaswa kuwa na sifa ya kuwezesha msawezo (balance) makinifu baina ya mambo hayo mawili.

 

                                     “ Enyi mlioamini kuweni wasimamizi (wa kupitisha haki) kwa ajili ya

                                     Mwenyezi Mungu, muwe mkiota Shahada kwa uadilifu..”  (Al- Maidah, 5:08)

 

“Enyi mlioamini! Kuweni wenye kusimamisha uadilifu mtoapo ushahidi

kwa ajili ya Mwenyezi Mungu; japokuwa ni juu ya nafsi zenu, au juu ya

wazazi (wenu) na jamaa (zenu)..” (An Nisaa, 4:135)

 

Kwa kuzingatia mafundisho ya uislam, uadilifu ni kanuni inayopaswa kuongoza mwenendo wa muislamu. Kwa kiongozi wa kiislam, kanuni hii ni ya muhimu zaidi kutokana na wajibu alionao kwa taasisi, jumuiya, asasi, ummah na watu wanaowaongoza. Pasipo kanuni hii, uonogzi wa kiongozi  utaingia dosari kubwa kitu ambacho kitzaa mdororo wa uonogozi

 

6.3  Ushujaa  na Ujasiri

Viongozi wanaposwa kuwa mfano kwa kudhihirisha ushujaa na ujasiri. Kiongozi hapaswi kuogopa kuikabili hatari. Ushujaa na ujasiri ni wasifu muhimu kwa kiongozi ili aweze kuwawezesha wafuasi wake kutekeleza jukumu lao hususan linapokuwa ni jukumu zito.

 

Mfano: katika vita vya Badr ushujaa na ujasiri wa Amir Jeshi, ni miongoni mwa mambo yaliyowezesha ushindi wa waislam katika viwanja vya Badr.

 

Wakati tawi linapokuwa likikabiliana na changamoto kadhaa zikiwemo njama dhidi ya Jumuiya ya kiislamu, ushujaa na ujasiri wa kiongozi ni miongoni mwa mambo muhimu kwa ajili ya tawi hilo kufanikiwa katika harakati zake. Katika uongozi wa TAMSA kuna mambo mengine ambayo ni ya hatari kwa maisha ya kiongozi kitaaluma, lakini kwa ajili ya uislamu na waisalamu, inampasa kiongozi ayakabili japokuwa yanaonekana ni ya hatari. Kiongozi wa TAMSA akikosa ushujaa na ujasiri, sio siri kwamba hatamudu kulikabili hili.

 

 

6.4                          Uamuzi  na Kuazimia

Kiongozi lazima asiwe mzito kutoa maamuzi iwapo kiongozi ni mzito kuamua, ataiweka taasisi, asasi au jumuiya anayoiongoza, katika hatari ya kuhasirika na kudorora.

“Uamuzi unaocheleweshwa unaweza kuwa fursa ya kuhasirika.”

(Zatar Bangash).

 

Mtume (s.a.w) hakuwa mzito kuamua hata wakati alipokuwa katika hali nzito. Mathalani: alikuwa mchukua uamuzi kwa wakati aliposhughulikia Banu Qaiynuka, Banu Nadhir na Banu Quraidha makabila haya yalikuwa na chokochoko na vitimbi dhidi ya Uislam na dola ya Kiislam.

 

6.5  Udhihirishaji dhamira

Kiongozi lazima aweze kudhihirisha dhamira yake. Hii ni pamoja na kuweza kuonyesha dhamira waziwazi na kuwavuta pamoja na kuwavuta watu katika dhamira hiyo kwa kuzingaia seerah ya Mtume (s.a.w) mara tu alipoanza kuutangaza uislam, alibainisha dhamira na kufanikiwa kuwavuta watu katika uislam mara moja. Hata wakati makafiri wa kiquraish walipomtuma Ut’bah Ibn Rabah kumpelekea Mtume (s.a.w) machaguo manne, ili kumfanya aache kuutangaza uislam, Mtume (s.a.w) alimsomea Ut’bah sura ya Ha mim sajda, (sura ya 41 ). Katika kukataa pendekezo la makafiri, Mtume (s.a.w) alifahamu kabisa kuwa uamuzi huo ungeongeza  madhila kwa waislam, lakini aliona pia kuwa kudhihirisha dhamira ilikuwa ni bora zaidi ya kutoridhisha. Kwamba kwa kutodhihirisha dhamira ingekuwa haifai, haifai hasa.  Ni kwa mantiki hiyo hiyo, pindi viongozi wa TAMSA mashuleni na vyoni wanapopewa maelekezo kutoka utawala, ambayo yanakinzana na matakwa ya uislam, wanapswa kudhihirisha kuwa hilo haliwezekani japokuwa wanadhani kufanya hivyo kutasababisha madhila.

 

7.0 UHUSIANO WA KIUTAWALA BAINA YA KIONGOZI NA WAFUASI

Ingawa kwa wakati wa sasa, Jumuiya na taasisi za kiislamu zina viongozi wanaitwa kwa vyeo  vizuri kama vile Amir, Amirah na vinginevyo, lakini hakuna ubishi kwamba kunatatizo la ki- uhusiano baina ya viongozi na wafuasi. Tatizo lipo katika uelewa wa viongozi na uelewa wa wafuasi. Madhumuni ya maudhui hii kugusa uhusiano baina ya kiongozi na wafuasi, haina maana kuwa wafuasi wawe na nidhamu za kibubusa kwa viongozi na wala sio maana yake kwamba wafuasi wasiwe na utii kwa kiongozi. Kubwa hapa ni kuwa hakuna uhusiano usio na mipaka. Uhusiano baina ya kiongozi na wafuasi unapaswa kudhihirishwa haraka sana mara tu mtu anapoanza uonogozi kwa muktadha huu maeneo mawili yataguswa.

7.1                         Utii

Suala muhimu la kuzingatia ni kwamba, kama uongozi ni wajibu, kwa nini utii usiwe wajibu? Pasipo utii ndani ya Jumuiya, Taasisi au jamii ni vigumu kufanikiwa. Iwapo hakuna utii ndani ya jumuiya au taasisi, kutakuwa na mashaka juu ya mfumo huo kuwa ni wa kiislamu.

 

Utii wa muislam kwa kiongozi wake ni amri ya mwenyezi Mungu.

 

“ Enyi mlioamini! Mtiini Mwenyezi Mungu, Mtiini Mutume

wake(s.a.w) na wale walio na mamlaka miongoni mwenu” (Q.4:59)

 

Mtume (s.a.w) amesisitiza sana utii kwa viongozi. Amesema mtume wa mwenyezi Mungu.

 

 “Yeyote anayenitii mimi, anamtii Allah (sw) na yeyote asiyenitii mimi

hamtii Allah (sw) na yeyote anayemtii kiongozi, ananitii mimi, na yeyote

asiyetii kiongozi basi hanitii mimi”[22]

 

Kwa kuzingatia Quran na Sunnah kama ilivyoelezwa hapo ju, basi kielelezo cha mamlaka na utii kinaweza kuwa kama ifuatavyo:-

Kielelezo cha mtitiriko katika utii

Text Box: MAMLAKA

MTUME

 
Text Box: UTII

KIONGOZI

 

WAFUASI

 
 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


Chanzo: Ufafanuzi wa mwandishi.

 

Mtume (s.a.w) alisema pia:

 

“Kusikia na kutii ni jukumu la muislamu kwa yeyote

anayopenda na asiyoyapenda”[23]

 

Uislam umehimiza sana utii kwa viongozi kiasi kwamba umekataza aina yoyote ya kutokuwa na utii isipokuwa tu pale ambapo imetakiwa kutokutii kwa mujibu wa sheria za kiislam.

 

     7.1.1  Mipaka ya utii.

  Pamoja na msisitizo juu ya utii kwa viongozi lakini pia uislam haukubali utii wa     

   kibubusa.[24]

 

Dkt Badawi na Dkt Beekun walipiga mfano wa tukio ambapo Seyydna Umar (r.a) alipendekeza kiasi cha mahari kiwekwe maalum katika harusi. Kiasi alichokisema hakikuwa kikiendana na sheria ya kiislam. Ukht mmoja akasimama na kumwambia. “ Umar muogope mwenyezi Mungu”. Aliposikia hoja  nzuri iliyoendana na Quran na Sunnah, Umar alibaini kosa lake na kusema kuwa ukht alikuwa sahihi, na tabia hii ya Umar ni kielelezo kwamba wafuasi hawapaswi, kupokea  maelekezo ya kiongozi  pasipo kutafakari, na pale ambapo wafuasi wanaona kiongozi amekosea, wanapaswa kumkosoa.

 

Mipaka ya utii ni pamoja na hii ifuatayo:-

(i)                  Kutowatii maasi

“ Wala msitii amri za wale maasi” (Q.21:151)

 

“Ambao wanafanya uharibifu tu katika ardhi wala hawaitengenezi” (Q.26:152)

 

 

(ii)               Hakuna utii wa kutokutii

                               Imam Ali (r.a) amesema:

 

“ Mjumbe wa Mwenyezi Mungu alituma skauti na kumfanya mmoja wa Ansar kuwa kiongozi. Akawataka wamtii na kumsikiliza. Haraka wakamuudhi kiongozi wao, naye akawaamrisha kukusanya kuni na kuzitia moto, kisha akawaambia, ‘hamkuambiwa na mtume (s.a.w) kumtii na kunisikiliza?’ Wakasema ‘Ndiyo!’ Kisha akawaamrisha waingie kwenye moto;  wakakataa kuingia kwenye moto. Walioporudi walimweleza mtume (s.a.w)  kilichotokea, naye akawaambia kuwa laiti wangeliingia kwenye moto wasingetoka tena. Haiwzekani kuwepo utii wa kutokutii”[25]

 

Hata katika swala  za jamaa, kama Imam anakosea, maamuma waking’amua, humkosoa na pindi akiendelea licha ya kukumbushwa watu hu-mkhalif Imam. Maelezo ya jumla ni  kuwa utii ni kwa ma’roof and wala si kwa munkar .

 

Baada ya kuona mipaka ya utii, suala linakuja :utii  ni kwa nani?

 

“Al- hadith

                    “ Msikilizeni na mtiini hata kama ni mtumwa kutoka Abysinia (uhabeshi[26]

 

 

8.0 HITIMISHO

 

“Tuongoze njia iliyonyooka, njia ya wale uliowaneemekea, sio ya wale

uliowaghadhibikia, wala wale waliopotea”.. (Q. 1:50-6)

 

Ni jukumu letu waislam, ni jukumu la viongozi wa waislam kutafuta njia iliyonyooka na kuifuata. Kuhusu sanaa na mchakto wa  uongozi, ipo njia iliyonyooka ambayo tunapaswa kuifuata sote.

 

Mafunzo yoyote, yawe Bungua bongo, darasa duara, semina au warsha yanapaswa kuwabadilisha watu katika mwelekeo (A), Stadi(s), maarifa (K) na uzoefu (E). Viongozi waliokutana  leo wanapaswa kujiuliza jipya walilopata katika shughuli hii. Tuendapo tukazingatie pamoja na mambo  mengine, hatua zifuatazo baada ya nukuu hii.

 

“ Kiongozi atakayeweza kufanikiwa ni yule atakayefikia malengo kwa

namna nzuri iwezekanayo, ikiwa ni  kwa kiwango chini kabisa cha

kutokuwa na ufaaji kwa anaowaongoza, tena kwa gharama za chini kabisa,

                         kwa wakati muafaka na kwa viwango bora vya utendaji “(Abdul Ghani Ahmed)[27]

 

Pamoja na mbinu za kisasa za uongozi, kuna namna nyingi ya kuliendea hilo, lakini njia iliyotumiwa na nabii Muhammad(s) (s.a.w) ni bora zaidi, kwa kuwa ilikuwa na mwongozo wa Allah (s.w.t)

 

         “Kwa hakika kutoka kwa mtume wa allah mnamfano wa kiga” (Q.33:21)

 

Kwa hiyo kiongozi azingatie

  1. Upole unaofaa

 

“ Mwenye uthabiti/ nguvu si yule ambaye anawashinga wenzaka

 kwa maguvu    ila ni yule ambaye ingawa amekasirka, anajidhibiti[28]

 

  1. Uwezo wa kulingania

 

“ Liwepo katika ninyi kundi ambalo litawalinganisa watu kufanya

                  mema, kusimamisha haki na kukataza mabaya. Watu hao ndio

watakaofanikiwa” (Q.3:104)

 

  1. Utunzaji ahadi na uaminifu

 

”Wale ambao kwa imani kubwa wanatunza uaminifu wao naahadi zao

          ndo watu wa peponi; humo watakaa milele.” (Q. 23:8)

 

 

 

  1. Uadilifu

 

“ Tuliwatuma mitume wetu pamoja na kuwapa mwongozo na vitabu na

vipimo vya ili wapate kusimamia uadilif “ (Q.57:25)

 

  1. Kuacha yasiyotuhusu.

 

“ Mtu atakamilika katika dini yake (Islam) pale ambapo ataacha

lisilomuhusu.” (Tirmidh)[29]

 

  1. Ukweli

 

“ Enyi miloamini mfuateni Mwenyezi Mungu na muwe pamoja na

wakweli” (Q. 9:119)

 

”Kuna ishara 3 za mnafiki.” Akisema anadaganya; akiahidi hatizimizi;

akiaminiwa husaliti uamini” (Imesimuliwa na Abu Huraira (n.q) [30]

 

  1. Juhudi za uanzilishi wa jambo.

 

                  “ Kila shughuli isiyoanza kwa kumtakasa Allah(s.w) haitofanikiwa”

(Abu Dawud)[31]

 

  1. Uwajibikaji

“ Kila mmoja wenu ni mwangalizi na anawajibika juu ya waliochini ya

 mamlaka yake. Mtawala ni mwangalizi na hivyo anao wajibu  juu ya

waliochini yake. Mwanamume anaowajibu juu ya familia yake na wote

 walio chinni ya uangalizi wake kwa namna hiyo hiyo kila mmoja wenu

 ni mwangalizi na mwenye wajibi kwa dhamana aliyonayo[32]

 

 

  1. Kujitolea

“ Hamtafikia uchamungu mpaka mtoe katika mnavyovipenda.

Na chochote manachotumia Mwenyezi Mungu anafahamu” (Q. 3:92)

 

  1. Kuwa katika timu

 

“ Na shikamaneni katika kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala

 msifarakane; na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu

yenu mlipokuwa maadaui, naye akaziunganisha nyoyo  zenu, hivyo

 kwa neema yake mkawa ndugu; na mlikuwa ukingoni mwa shimo la

moto naye akawaokoeni. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu

anavyokubainishieni Aya zake ili mpate kuongoka. (Q. 3:103) [33]

 

  1. Kuongozana

 

“ Wakati watu watatu wanondoka kwenda safari, wamchague

 mmoja wao kuwa kiongozi”[34]

 

12. Kuwa katika Timu

                                “ Waumini wa kweli miongoni mwao ni kama tofali za ukuta,

                               zinakamatana na kushikamana hasa kila moja, aliposema hivyo

                          Mtume (s.a.w) alishikamanisha vidole vya mikono yake (Interlocking)[35]

 

 

MWISHO

 

WA BILLAH TAWFIQ

ALLAH NDIYE MJUZI WA YOTE



[1] Tanzania Problems faced by Da’wah and the D a’iyah, uk.77

 

[2] Fasiri iliyotolewa na Dr. Badawi katika warsha iliyofanyika kwalalumpa, Tarbiya and Training Centre, International Islamic University, Malasia, 1998.

[3] Taz. Training Guide for Islamic workers, Dkt. Hisham (1993) uk. 50

[4] Taz.    Sunnah al Tirmith, Sunnah Abu Dawud, Sahili al Muslim, Sahih al Bukhar.

[5] Taz.Omar Hassan Kasule, Sr. Leadership Module, General theme: Leadership. Workship 1. In muslim leaders’ forum 98 Handbook. (kuala Lumpur, Malaysia: Tarbiyyah and Training Center, Internation Islamic university Malaysia, 1993.

[6] Taz. Mwito kwa waislamu kuimarisha umoja wao – Mwinyi, 1988, uk.10

[7] Taz. The leadership process in Islam, Beekun and Badawi, uk. 3, 1999

[8]  Taz. Beekun and Badawi (1999) the leadership process in Islam,  p.3

[9] Badawi Anarejea sahihi Muslim, volume 3, 1013.

[10] Taz. Dkt. Badawi (k.h.j.) Uk 4 .

[11] Khalifa wa pila katika Uislam

[12] Sahihi Bukhar, volume 9, hadith 259, sahihi Bukhar vol. 5, hadith 629 kama ilivyorejewa na Dkt. Badawi (kh.j)

[13] Taz. Muhammad Al Buraey. Administrative development: An Islamic perspective (London , U.K.: KPI, 1985),248

[14] Imeelezwa hivyo na Dkt Badawi katika makala aliyoandika kwa kushirikiana na Dkt Beekun, 1999 uk.   

    

[15] Naceur Jabnourn, Islam and Management, 1994 uk. 6

[16] Taz. Sayyid Abu  A’ la maudodi: The Islamic movement: dynamics of values, power and change . uk. The Islamic foundation, 1991, p. 115

[17] Taz. Behzadnia and Denny: To the commander in chief: form Iman Ali to malik –E- Ashter (1981)p.8

[18] Quran sura ya 16 aya ya 90

[19] Nukuu ya Dkt Badawi, ni Sahihi Muslim, hadith 1:47

[20] Taz. http://www. Islamicthought. Org/ pp- 26 – leader. Html. The Concept of leader and leadership by Zafar Bangash.

 

[21] Taz. Zafar Bangash, (khj, uk. Wa 6)

[22] Taz. Al – Bukhar na Muslim

[23] Amesimulia Ibn Umar, tazama Rahman, 75

[24] Taz. Badawi and Beekun (1999) The leadership process in Islam, uk 16

[25] Taz. Fathi Yakan, problems facing da’ awah and daiyah, uk. 88

[26] Sahihi Muslim na Sahih Bukhar

[27] Taz. A – Z steps to leadership in Islam, htt://www. Geocities.com multmainaa/takkur/leadership –

    Islamic htm/?2006 24/4/2006

[28] Hadith kutoka sahihi – al Bukhar

[29] Imenukuliwa na Abdul Ghani Ahamed Barrie (khj)

[30] Khj

[31] Tafsiri ya mwandishi, kutoka khj

[32] Taz. Htt:/ www. Geocities. Com/mutmainaa/tafakkr/leadership- Islam. Html? 2000624

[33] Khj

[34] Taz. Dibaji iliyoandikwa na Sheikh Ramadhan Tahir Mpendu wa BALUKTA – 3/9/1988 Mwito Kwa Waislam Kuimarisha Umoja Wao

[35] Abdul Ghani anarejea shih al Bukhar